2 Chronicles 4:1-6

Vifaa Vya Hekalu

(1 Wafalme 7:23-51)

1 aMfalme Sulemani akatengeneza madhabahu ya shaba yenye urefu wa dhiraa ishirini,
Dhiraa 20 ni sawa na mita 9.
upana wa dhiraa ishirini na kimo chake dhiraa kumi.
Dhiraa 10 ni sawa na mita 4.5.
2 dAkatengeneza Bahari ya kusubu, yenye umbo la mviringo, ya dhiraa kumi kutoka ukingo hadi ukingo na kimo cha dhiraa tano. Kamba ya urefu wa dhiraa thelathini
Dhiraa 30 ni sawa na mita 13.5.
ingeweza kuizunguka.
3 fChini ya huo ukingo, kulikuwa na mafahali kuizunguka, yaani mafahali kumi katika kila dhiraa moja.
Dhiraa moja ni sawa na sentimita 45.
Hayo mafahali waliyasubu katika safu mbili yakiwa ya kitu kimoja na hiyo Bahari.

4 hBahari hiyo ilikaa juu ya mafahali kumi na wawili, mafahali watatu walielekeza nyuso zao kaskazini, watatu magharibi, watatu kusini na watatu mashariki. Bahari hiyo ilikaa juu ya hao mafahali, nazo sehemu zao za nyuma zilielekeana. 5 iUnene wake ulikuwa nyanda nne,
Nyanda nne ni sawa na sentimita 7.5.
na ukingo wake ulifanana na ukingo wa kikombe, kama ua la yungiyungi iliyochanua. Iliweza kuchukua bathi 3,000.
Bathi 3,000 ni sawa na lita 60,000.

6 lKisha akatengeneza masinia kumi kwa ajili ya kuoshea vifaa, naye akayaweka matano upande wa kusini na matano upande wa kaskazini. Ndani yake ndimo walioshea vifaa vya kutumika katika sadaka za kuteketezwa, lakini ile Bahari ilikuwa ni kwa ajili ya makuhani kunawia.

Copyright information for SwhKC